Wakili wa serikali Dk.Tulia Ackson akifanya mahojiano na wanahabari
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania leo imehairisha
tena kesi namba 37 ya mwaka huu, ya mlalamikaji kuiomba mahakama itoe
tafsiri ya kifungu cha 104 kidogo cha (1) cha Sheria ya Uchaguzi kama
kinazuia ama la wananchi kukaa umbali wa mita 200 baada ya kupiga kura
katika vituo.
Kesi hiyo sasa itatolewa maamuzi maalum kesho saa 4 asubuhi.
Katika kesi hiyo, mawakili wa serikali
wanaongozwa na Naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali, Dk.Tulia Ackson huku
upande wa mlalamikaji ukiongozwa na Peter Kibatala.
Shauri hilo lililofunguliwa na Mgombea
Ubunge Viti Maalumu Jimbo la Kilombero (Chadema), Amy Kibatala, akitaka
mahakama hiyo itoe tafsiri sahihi ya kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya
Uchaguzi.

Note: Only a member of this blog may post a comment.