Miss Tanzania 2007, Richa Adhia.
Stori: Imelda Mtema
VUNJA ukimya! Miss Tanzania 2007, Richa Adhia ambaye amevunja rekodi
kwa kutokuwa na skendo tangu anyakue taji hilo, amefunguka kwa mara ya
kwanza kuhusiana na ndoa yake ambayo alikuwa akitarajia kuifunga
ughaibuni na mchumba wake wa muda mrefu, Hridhaan Dhllon.
Akizungumza na gazeti hili, Richa alisema kuwa kila kitu kilienda
sawa lakini kukawa na kikwazo kimoja kikubwa cha yeye baada ya kufunga
ndoa kwenda kuishi nje na mumewe, jambo ambalo lilikuwa gumu kwake. “Taratibu zote zilikamilika lakini
tulishindwana sehemu ya kuishi.Yeye alitaka tukaishi nje lakini
ilishindikana hivyo na ndoa ikayeyuka, tumebaki marafiki tu wa kawaida,”
alisema Richa.
Note: Only a member of this blog may post a comment.