Chama cha wamiliki wa mabasi nchini (TABOA)
kimeamua kusitisha huduma zake zote siku ya October 25, ili kuwaruhusu
madereva wake kupata nafasi ya kupiga kura katiaka kuchagua viongozi
watao wafaa.
Akizungumza na wanahabari mapema hii
leo, muweka azima wa chama hicho bw. Issa Nkya amesema kwamba wanatambua
kuwa wafanyakazi wao nao wanatakiwa kuungana na wananchi wengine katika
kupiga kura.
“Sisi
kama TABOA tumejipanga kuwapa ruksa wafanya kazi wetu ili kila mtu
akapige kura kwakuwa ni jambo la msingi kwa kumchagua mtu atayemtaka.:- Issa
Naye mwenyekiti wa chama cha
wasafirishaji mkoani Kilimanjaro na Arusha Bw. Mohamed Alfa amewataka
madereva kuhakikisha kuwa wanaongeza umakini katika kupiga kura ili
kuepusha uwezekano wa kutokea kwa vurugu.
“kwanza
kabisa tunawahasa mafanyakazi wetu tunawahasa kuepukana na ushabiki,
dereva awe ni mtulivu na kuwa sehemu ya kuleta amani na ikitokea
mabishano awaelimishe kwamba kila mtu kuwa na chama siyo uadui”
Bonyeza play kusikiliza mahojiano haya

Note: Only a member of this blog may post a comment.