Gladness Mallya
STAA wa filamu Bongo, Tiko Hassan amemuomba Mungu
aiepushe Tanzania na machafuko wakati huu taifa likijiandaa kwa uchaguzi
mkuu wa rais, wabunge na madiwani hapo Oktoba mwaka huu.
Staa wa filamu Bongo, Tiko Hassan.
Akipiga stori na gazeti hili, msanii huyo aliwataka watu kutofanya
mambo kwa kufuata mkumbo kwani uchaguzi unaonekana kuwa mgumu wenye
mchuano mkali baina ya vyama vyote vya siasa.“Nina wasiwasi sana na uchaguzi wa mwaka huu, kwani lolote linaweza kutokea, hivyo Watanzania wanatakiwa kuwa makini na kuachana na tabia ya kufuata mkumbo kwani hali inavyoonekana tusipokuwa makini vurugu zinaweza kutokea hivyo tumuombe Mungu sana,” alisema Tiko.

Note: Only a member of this blog may post a comment.