Musa Mateja
HUZUNI! Mtangazaji mahiri wa
Kituo cha Televisheni cha Star TV, Sauda Mwilima hivi karibuni alipatwa
na majonzi mazito baada ya kujifungua mtoto kwa upasuaji ambaye kesho
yake alipoteza maisha, akimuacha akiwa hoi kitandani.
Hii ni mara ya pili kwa mtangazaji huyo
wa habari za burudani kutokewa na jambo hilo, kwani miaka michache
iliyopita aliwahi kujifungua mtoto ambaye naye alifariki. Katika tukio
la juzi, mtoto huyo aliyekuwa wa kike, alizaliwa akiwa na umri wa miezi
saba.
“Alijifungua Jumatano iliyopita na kesho
yake mtoto akafariki, mimba ya kwanza nayo alijifungua mtoto wa kiume
lakini haikuwa bahati, tumeumia ila tunamshukuru Mungu kwa kuwa mke
wangu hajambo,” alisema Best.

Note: Only a member of this blog may post a comment.