Wakati kampeni za uchaguzi mkuu zinaendelea, wagombea wameendelea kutoa ahadi zinazolenga moja kwa moja matakwa ya wananchi katika maeneo mbalimbali ambapo jana mgombea urais kupitia Chadema, Edward Lowassa aliwagusa wakazi wa Morogoro.
“Lakini ninaamini hilo suala linawezekana, kukitaifisha kiwanda hiki kuwa kiwanda cha umma,” alisema.
Katika hatua nyingine, Lowassa aliwaahidi wananchi hao kuwa atahakikisha serikali yake inakuwa serikali rafiki ya wananchi wa kima cha chini hususan mama ntilie, bodaboda na wafanyakazi wadogowadogo huku akiisisitiza ahadi yake ya kuanzisha benki yao.
Kadhalika, Lowassa alisema kuwa ahadi ya serikali yake kuwa itatoa elimu bure kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu itazingatia utoaji wa elimu bora na sio bora elimu.

Note: Only a member of this blog may post a comment.