Wednesday, September 23, 2015

Anonymous

List ya Wachezaji Wanaolipwa Mishahara Mikubwa Ligi Kuu Marekani, Gerrard, Kaka na Wengineo Ipo Hapa...


Tumezoea kusikia mishahara ya wachezaji soka barani Ulaya kuwa mikubwa ila wengi wamekuwa wakijiuliza kwa nini mastaa kadhaa kutoka Ulaya wamekuwa wakikimbilia Ligi Kuu Marekani (MLS)? wengine usema wanafuata mishahara wengine usema Ligi Kuu Marekani (MLS) ni Ligi ya wastaafu.

September 23 nakuletea list ya mishahara ya mastaa wa soka waliowahi kucheza soka katika Ligi mbalimbali pendwa barani Ulaya, huenda ulitamani kujua mshahara wa mchezaji bora wa Dunia Ballon d’Or wa mwaka 2007 Ricardo Kaka ambaye amewahi kutamba katika vilabu vya AC Milan na Real Madrid.
Nakusogezea list ambayo imeandikwa na mtandao wa metro.co.uk ya wachezaji wanaolipwa fedha nyingi katika Ligi Kuu Marekani.

1- Ricardo Kaka

Ricardo Kaka analipwa mshahara wa dola milioni 6.6 na klabu yake ya Orlando City kwa mwaka.

2- Steven Gerrard

Steven Gerrard anayeitumikia klabu ya LA Galaxy analipwa mshahara wa dola milioni 6.2 kwa mwaka.

3- Frank Lampard

Kiungo wa zamani wa klabu ya Chelsea ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya New York City FC Frank Lampard analipwa dola milioni 6 kwa mwaka.

4- Michael Bradley

Michael Bradley anayecheza klabu ya Toronto FC analipwa sawa na Lampard dola milioni 6 kwa mwaka.

5- David Villa

David Villa wa klabu ya New York City analipwa dola milioni 5.61

6- Sebastian Giovinco

Sebastian Giovinco analipwa na klabu yake ya Toronto dola milioni 5.6.

7- Jozy Altidore,

Jozy Altidore analipwa dola milioni 4.75 kwa mwaka katika klabu ya Toronto FC .

8- Robbie Keane

Robbie Keane wa LA Galaxy analipwa dola milioni 4.5 kwa mwaka.

9- Giovani Dos Santos


Giovani Dos Santos wa LA Galaxy analipwa dola milioni 4 kwa mwaka

10- Clint Dempsey

Clint Dempsey kutokea klabu ya Seattle Sounders analipwa dola milioni 3.9.
Hii ni list ya wachezaji wote 18 wanaolipwa fedha nyingi na vilabu vyao katika Ligi Kuu Marekani (MLS)

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.