Saturday, September 19, 2015

Anonymous

DUNIA INA MAMBO: Ndoa Imefungwa Fastafasta Beach, Mtu na Mpenziwe...Waalikwa ni Watu Nane tu! (+PICHAZ)

Ronke na Lawson wamependana? Love yao hawakutaka masuala ya kusumbuana na ndugu masuala ya michango, vikao vya Harusi, kujaza watu Ukumbini.. wao kila kitu kimefanywa simple tu yani.
Jumapili ya September 13 2015 mambo yalikuwa motomoto kwenye Beach moja Lagos Nigeria, Ronke na Lawson walifunga Ndoa yao kwa mtindo wa aina yao kabisa yani !!
Ndoa ilifungwa kwa wapenzi hao kula viapo walivyobuni hapohapo tena wao wenyewe, hakuna pete wala Mchungaji wa kufungisha Ndoa… Badala ya pete, Bibi Harusi alivalishwa cheni ya dhahabu na mumewe, bwana harusi nae akavalishwa soksi na mkewe, mambo yakaendelea !!

Beach-wedding-one-300x232
Wageni waalikwa list hata haikuwa ya kuumiza vichwa, walialikwa ni watu nane tu… unaambiwa kwenye hao nane na mpiga picha nae kahesabiwa humohumo.
Beach-wedding-three-254x300
Beach-wedding-two-300x225
Mambo ya After Party je ??? Iliishia hivi, bibi harusi na bwana harusi walijiachia kwenye maji wakaogelea alafu mambo ndio yameisha hivyo, Bibi na Bwana wanaendelea na maisha mdogomdogo !!
Beach-wedding-six-300x204
Dunia ina mambo yake mdau, unatamani na wewe ungeishuhudia hii mdau wangu??

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.