Thursday, September 24, 2015

Anonymous

Chama cha ACT Wazalendo Wamejibu Kwenye Sentensi Tisa Kuhusu Utafiti wa TWAWEZA… (Audio)

Siku chache baada ya Taasisi ya TWAWEZA kutoa Ripoti ya Utafiti waliofanya kuelekea Uchaguzi Mkuu Tanzania, October 25 2015… Viongozi wa Vyama mbalimbali wametoa misimamo yao kuhusu Utafiti huo. 

Jana September 23 2015 January Makamba alitoa Taarifa kuhusu msimamo wa CCM kwenye Utafiti huo, ninakusogezea na hii pia mtu wangu, Taarifa kutoka Makao Makuu ya ACT- Wazalendo Dar es Salaam. 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kampeni wa Chama cha ACT-Wazalendo, Nickson Tugala alitoa taarifa hiyo >>> Chama cha ACT kimeyapokea na kuyapitia Matokeo ya utafiti uliofanywa na TWAWEZA… Utafiti unaonesha Ilani ya ACT imezingatia mahitaji ya Watanzania“>>>
ACT tunafarijika kwamba Chama chetu ni Chama pekee nje ya CCM na UKAWA kilichotajwa na Wapigakura zaidi ya Asilimia moja, kimekuwa chama cha nne katika kukubalika kwa Wapigakura nyuma ya CCM CHADEMA na CUF” >>> Nickson Tugala.
Screen Shot 2015-09-24 at 12.04.43 PM
Nickson Tugala 
Takwimu hizo zilikusanywa wakati ambao ACT-Wazalendo hakijamtangaza Mgombea wake wa Urais wala tulikuwa hatujafanya Uzinduzi wa Kampeni… Kama Utafiti huu ukirudiwa tunaamini tutafanya vizuri zaidi” >>> Nickson Tugala.
Screen Shot 2015-09-24 at 12.04.54 PM
Sauti yenye Taarifa yote hii hapa chini mtu wangu, Ripoti kutoka Makao Makuu ya ACT- Wazalendo Dar es Salaam.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.