Saturday, August 1, 2015

Anonymous

Usajili wa MESSI Coastal wazua Utata!

Na Omary Mdose
COASTAL Union imetangaza kumsajili kiungo wa zamani wa Simba, Ibrahim Twaha ‘Messi’ kwa mkataba wa miaka miwili, utata umeibuka juu ya usajili huo.
Mmoja wa marafiki wa karibu wa Messi aliliambia gazeti hili kwamba, kiungo huyo amesaini mkataba wa miezi minane tu kisha aende Afrika Kusini kucheza soka la kulipwa.
“Viongozi wanatangaza Messi kasajiliwa na Coastal miaka miwili, siyo kweli kwani ukweli ni miezi minane tu kwani anataka kwenda kujiunga na klabu moja huko Afrika Kusini,” alisema rafiki huyo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.