Saturday, August 1, 2015

Anonymous

USAJILI VPL: Sherman ambakiza Coutinho YANGA SC

sherman
Na Omary Mdose
STRAIKA wa Yanga aliyetimkia nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kukamilisha dili la kucheza soka nchini humo, Mliberia, Kpah Sherman, dili lake limekuwa nafuu kwa kiungo wa timu hiyo, Mbrazili, Andrey Coutinho aliyekuwa akitaka kutolewa kwa mkopo.

Sherman aliyeondoka hivi karibuni, muda wowote kuanzia sasa anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya kabla ya kupewa mkataba wa kuitumikia Klabu ya Mpumalanga inayoshiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini (PSL).

Mara kwa mara imeripotiwa kwamba, wachezaji kadhaa wa Yanga walikuwa kwenye mipango ya kutolewa kwa mkopo kwenye timu mbalimbali ambapo jina la Coutinho lilikuwa miongoni mwa hayo huku mchezaji huyo akionekana kutokuwa tayari kwa hilo.

Klabu zilizoonyesha nia ya kuihitaji huduma ya Mbrazili huyo zilikuwa ni St. George ya Ethiopia na FC Platinum ya Zimbabwe ambapo kwa sasa dili hilo limesitishwa kutokana na kwamba Yanga imebakiwa na nafasi moja ya mchezaji wa kimataifa.

Taarifa kutoka katika benchi hilo la ufundi linaloongozwa na Mholanzi, Hans van Der Pluijm, zinasema kwamba kwa sasa dili la kumtoa kwa mkopo Coutinho wamelisitisha kutokana na kuondokewa na Sherman huku wakiwa na nafasi moja ya mchezaji wa kimataifa.

“Kwa sasa uongozi umesitisha lile zoezi la kumtoa kwa mkopo Coutinho kutokana na kwamba Sherman ameondoka hivyo pengo lake wanaangalia watalizibaje, lakini hiyo imechagizwa na mchezaji mwenyewe kutokana na kung’ang’ania kubaki huku akiahidi kuipa mataji timu yake,” ilieleza taarifa hiyo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.