Rapa wa kike aliyejizolea umaarufu kutoka lebo ya Cash Money, Nicki Minaj.
Burgettstown, Pennsylvania
RAPA wa kike aliyejizolea umaarufu kutoka lebo ya Cash Money, Nicki Minaj hivi karibuni ametangaza kuwa ni mjamzito.
Nicki (32) aliweka wazi alipokuwa jukwaani katika tamasha kubwa
lililojumuisha ziara yake ijulikanayo kama Pinkprint huko Pennsylvania
ambapo alipanda na mchumba wake, Meek Mill na kusema;
“Piga kelele kwa baba wa mtoto wangu!”
“Piga kelele kwa baba wa mtoto wangu!”
Baada ya shoo hiyo, kupitia ukurasa wake wa Twitter, Nicki aliweka
kipande cha video hiyo akizungumza maneno hayohayo sambamba na
kuambatanisha kikatuni (emoji) ya kulia.
Kwa kipindi kirefu Nicki amekuwa na uhusiano na Meek Mill ambapo hivi
karibuni uhusiano wao ulidaiwa kuteterereka kwa kile kilichoelezwa ni
kutupiana matusi kwa Meek na Drake kwenye nyimbo zao na mitandao ya
kijamii.
Hongera Nicki kwa ujauzito ulionao!
(Imeandaliwa na Andrew Carlos kwa msaada wa mtandao)

Note: Only a member of this blog may post a comment.