Tuesday, August 18, 2015

Anonymous

MSHTUKO MKUBWA! Gonjwa la AJABU Laibuka Jijini Dar...Wawili Wameshafariki Ghafla!

sanchawa1 
Haruni Sanchawa na Makongoro Oging’
Mshituko mkubwa umewakumba wakazi wa Kijitonyama Kwaally Maua B, wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam baada ya Ijumaa kuamkia Jumamosi iliyopita kuibuka kwa ugonjwa wa ajabu ulioua watu wawili ghafla na kuwapa hofu kubwa wakazi wa eneo hilo.
IMG_0132
Timu ya Uwazi baada ya kuarifiwa juu ya tukio hilo, ilifika katika eneo hilo na kukuta wafiwa wakilia huku wagonjwa wengine wakikimbizwa hospitalini.
Katika mahojiano na mjumbe wa shina namba 19 wa eneo hilo, Mohamed Juma Ngaopera alisema tatizo hilo lilianza Ijumaa iliyopita saa 3.30 usiku.
IMG_0137“Hatujajua chanzo lakini ugonjwa ulikuja ghafla kwa watu kuugua tumbo ambapo watoto walikuwa wakilia sana na baadaye kuanza kuharisha, mtoto mmoja akafariki dunia.
 “Ugonjwa huo ukaenea eneo hili na waliokuwa wakikumbwa tukawa tunawakimbiza hospitalini lakini mtu mzima mmoja naye akafariki hivyo, mpaka sasa watu wawili wameshapoteza  maisha,” alisema kiongozi huyo.
Alipoulizwa chanzo, alisema hawajui kwa sababu haujabainishwa kitaalamu na amewataja waliopeteza maisha kuwa ni Zawadi Kipepe (5) na Abas Hussein (50).
IMG_0140 
Alisema baadhi ya wagonjwa waliokumbwa na maradhi hayo na wanaendelea na matibabu ni pamoja na Ramadhan Hussein, Shaban Hussein, Saum Kipepe, Idrisa Kipepe, Morina Mohamed  wote wamelazwa Hospitali ya Parestina, jijini Dar. 

Kiongozi huyo aliongeza kuwa, baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya waliomba msaada Halmashauri ya Jiji ambao walifika na kupuliza dawa eneo hilo kisha kufunga nyumba ambazo wagonjwa hao walikuwa wakiishi ili uchunguzi zaidi ufanyike. 

Hata hivyo, mmoja wa maafisa wa afya wa jiji waliofika eneo hilo alipoulizwa na waandishi wetu kama dalili za ugonjwa huo ni za kipindupindu, kwa sharti la kutoandikwa jina kwa kuwa siyo msemaji, afisa huyo alisema:

 “Kinachoonekana hapa si kipindupindu bali kuna uhasama kati ya familia moja na nyingine. Kwa  nini tatizo hilo liikumbe familia moja tu?”

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.