JIJI la Dar es Salaam na vitongoji vyake, leo lilisimama kwa muda baada ya mgombea wa nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Pombe Magufuli na mgombea mwenza, Samiah Suluhu Hassan kwenda katika ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuchukua fomu kwa ajili ya nafasi hizo.
Wagombea hao ambao wamesababisha mtikisiko mkubwa, walipitia Barabara ya Morogoro, Bibi Titi Mohamed na Ohio kuelekea katika ofisi hizo wakitokea Ofisi za CCM, Lumumba ambapo shughuli kadhaa za watu zilisimama kwa ajili ya tukio hilo huku pia wakionekana kivutio na wananchi kusikika wananchi wakiimba nyimbo mbalimbali.
Mbali na uchukuaji fomu, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dk Jakaya Mrisho Kikwete alifika katika ofisi ndogo za chama hicho kwa ajili ya kuwalaki wagombea hao.Rais Kikwete akisema kwamba CCM itarajie ushindi wa kishindo ifikapo Oktoba 25, mwaka huu.
Wapinzani watarajie anguko na pia ushindi mkubwa kwetu,” alisema Kikwete huku akishangiliwa na umati mkubwa wa watu.
Wagombea hao ambao wamesababisha mtikisiko mkubwa, walipitia Barabara ya Morogoro, Bibi Titi Mohamed na Ohio kuelekea katika ofisi hizo wakitokea Ofisi za CCM, Lumumba ambapo shughuli kadhaa za watu zilisimama kwa ajili ya tukio hilo huku pia wakionekana kivutio na wananchi kusikika wananchi wakiimba nyimbo mbalimbali.
Mbali na uchukuaji fomu, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dk Jakaya Mrisho Kikwete alifika katika ofisi ndogo za chama hicho kwa ajili ya kuwalaki wagombea hao.Rais Kikwete akisema kwamba CCM itarajie ushindi wa kishindo ifikapo Oktoba 25, mwaka huu.
Wapinzani watarajie anguko na pia ushindi mkubwa kwetu,” alisema Kikwete huku akishangiliwa na umati mkubwa wa watu.
(HABARI/PICHA : DENIS MTIMA NA HARUNI SANCHAWA/GPL)

Note: Only a member of this blog may post a comment.