Hans Mloli, Dar es Salaam
SUALA la kupata straika mpya atakayeisaidia Simba msimu ujao limezidi kumtesa Kocha Mkuu wa Simba, Dylan Kerr, ambapo sasa ameamua kufanya maamuzi magumu.
Kerr, raia wa Uingereza, amesema kuwa kama hatapata straika mpaka dirisha la usajili litakapofungwa, atakachokifanya kama mbinu yake ya pili ni kuwatumia wachezaji wake haohao waliopo, kuwabadilisha ili wafanye vile anavyotaka yeye katika suala la ufungaji mabao.
Kerr amekuwa akisisitiza kuwa mastraika alionao sasa, Mganda, Hamis Kiiza, Musa Hassan Mgosi, Ibrahim Ajibu wakisaidiana na Simon Sserunkuma bado hawajatosha kukamilisha makali ya safu hiyo kuelekea msimu ujao.
“Unafikiri nitafanya nini sasa kama dirisha litafungwa halafu sijapata straika? (anatabasamu) Itabidi niangalie kama kutakuwa na mtu mwingine anacheza nafasi ya tofauti na ana uwezo wa kufunga, tumuongezee baadhi ya vitu ili asaidiane na wenzake,” alisema Kerr.
Mpaka sasa zimesalia siku tisa pekee kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kimataifa, Septemba 6 na Ligi Kuu Bara inatarajiwa kuanza Septemba 12, mwaka huu.
Kerr, raia wa Uingereza, amesema kuwa kama hatapata straika mpaka dirisha la usajili litakapofungwa, atakachokifanya kama mbinu yake ya pili ni kuwatumia wachezaji wake haohao waliopo, kuwabadilisha ili wafanye vile anavyotaka yeye katika suala la ufungaji mabao.
Kerr amekuwa akisisitiza kuwa mastraika alionao sasa, Mganda, Hamis Kiiza, Musa Hassan Mgosi, Ibrahim Ajibu wakisaidiana na Simon Sserunkuma bado hawajatosha kukamilisha makali ya safu hiyo kuelekea msimu ujao.
“Unafikiri nitafanya nini sasa kama dirisha litafungwa halafu sijapata straika? (anatabasamu) Itabidi niangalie kama kutakuwa na mtu mwingine anacheza nafasi ya tofauti na ana uwezo wa kufunga, tumuongezee baadhi ya vitu ili asaidiane na wenzake,” alisema Kerr.
Mpaka sasa zimesalia siku tisa pekee kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kimataifa, Septemba 6 na Ligi Kuu Bara inatarajiwa kuanza Septemba 12, mwaka huu.

Note: Only a member of this blog may post a comment.