Tuesday, August 11, 2015

Anonymous

JUMA KASEJA Alipelekwa Oman na Viongozi wa SIMBA SC? Nini Kinaendelea?! Majibu Yapo Hapa...

Baada ya kuenea kwa uvumi wa muda mrefu kuhusiana na klabu ya Soka ya Simba kutaka kumrejesha kikosini golikipa wake wa zamani ambae alikuwa Yanga kabla ya kutibuana na viongozi wa klabu hiyo, Juma Kaseja team yetu ilibidi imtafute  kufanya exclusive interview na Kaseja.
juma-kaseja
Juma Kaseja ni golikipa aliyeichezea Simba kwa mafanikio kwa zaidi ya miaka saba ila sasa yupo kama mchezaji huru licha ya taarifa za awali kusambaa kuwa Kaseja kapelekwa Oman na baadhi ya viongozi wa Simba iliakajifue nakuja kuongeza nguvu kikosini, kabla ya taarifa nyingine kusema kuwa viongozi wa Simba wanavutana wapo wanaopenda arudi na wengine wanapinga. 

“Watanzania tumekuwa tukiongea sana kuliko vitendo mimi nafikiri Simba wana magolikipa wao ambao wamewasajili sasa ingekuwa ni ajabu kumchukua golikipa ambae hamjamsajili mnampeleka kwenda kufanya mazoezi ya maandalizi halafu wale mliowasajili mnawaacha”>>>Kaseja 

“Sijaenda Oman, sikuwa Oman na wala sikuwa ndani ya nchi hii nilikuwa nje ya nchi lakini nilichokifuata sipendi watu wajue ni maisha yangu binafsi”>>>Kaseja
Zaidi msikilize Kaseja akikupa kiini cha tatizo la yeye kuachwa Simba

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.