Friday, August 7, 2015

Anonymous

Hiki ndicho kipaji kingine cha Haruna NIYONZIMA wa YANGA SC

Kiungo wa kimataifa wa Rwanda anaekipa katika klabu ya Dar Es Salaam Young African (Yanga) Haruna Niyonzima August 7 amezungumza na team ya millardayo.com  kitu gani kingine ambacho anaweza kufanya kwa ufasaha zaidi ya mchezo wa mpira wa miguu.
haruna-niyonzima
Niyonzima ambae huwa ana uwezo mkubwa Uwanjani amesema anaweza kuimba muziki kwa ufasaha na tayari kaimba nyimbo tatu kati ya hizo zinapigwa kwao, ila anakiri kupenda kuimba na hawezi jua muziki unaweza utamfikisha wapi licha ya kukiri kuwa anafanya kwa kujifurahisha tu. 

“Kiukweli napenda mpira ni kipaji lakini after football sometimes napenda kuimba naamini pia nikiingia naweza kuimba sababu nishawahi kufanya majaribio, nikisema nimejaribu kuimba ni kwamba nimeenda studio na sasa hivi na nyimbo kama tatu”>>>Niyonzima 

Ikumbukwe kuwa Haruna Niyonzima amejiunga na Yanga mwaka 2011 akitokea katika klabu ya APR ya Rwanda, Niyonzima ambae ni mahiri uwanjani amebahatika kupata watoto wakike  mapacha  Atika na Atifa April 17 2015.
Nimekusogezea sehemu ya Interview na wimbo aliomuimbia mama yake hapo chini!

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.