Tuesday, August 18, 2015

Anonymous

FAHAMU Vyakula 7 Ambavyo Haviwekwi Kwenye Friji

Inajulikana kwamba ili chakula kikae kwa muda mrefu bila kuharibika, hasa matunda na mboga za majani, ni lazima kihifadhiwe sehemu yenye ubaridi, kama vile kwenye jokofu (friji). Lakini tafiti za kitaalamu zimebaini kuwa baadhi ya vyakula havifai kuhifadhiwa kwenye friji na kwa kufanya hivyo hupoteza ubora na kuharibika.
Katika makala haya, tunakuletea orodha ya vyakula saba ambavyo havitakiwi kuhifadhiwa kwenye jokofu:
How healthy are bananas? Bananas are rich in Vitamin B6 and a good source of fiber, vitamin c, magnesium and potassium.
NDIZI MBIVU: Ubora wa tunda hili huongezeka kadiri linavyoendelea kuiva. Virutubisho vinavyopatikana kwenye ndizi iliyoiva kidogo, iliyoiva kiasi na ile iliyoiva sana, vinatofautiana. Ili ndizi iendelee kuiva inahitaji kukaa kwenye joto la kawaida, unapoiweka kwenye baridi la kwenye jokofu, haiwezi kuendelea kuiva hivyo kuwa na virutubisho hafifu.
3I6XqnuyJuCNJwy4GefJqVo2VIAZI VITAMU: Utafiti unaonesha kuwa viazi vitamu vinapohifadhiwa kwenye jokofu, virutubisho aina ya wanga vinavyopatikana kwenye viazi hugeuka na kuwa sukari na huvuruga ladha yake ya asili, bila kusahau kwamba kiwango cha sukari kilichomo huongezeka mara dufu.
tomatoesNYANYA: Bila shaka wengi wetu tuna mazoea ya kuhifadhi nyanya kwenye jokofu kwa kuwa zinaweza kukaa kwa muda mrefu bila kuharibika, lakini ukweli ni kwamba nyanya inapowekwa kwenye jokofu hupoteza ladha na ikikaa kwa muda mrefu hubaki makapi tu.

TUFAHA: Kwa lugha maarufu, tunda hili linajulikana kama Apple, nalo kama ilivyo kwa nyanya, linapokaa kwa muda mrefu kwenye jokofu, hupoteza ladha na baadhi ya virutubisho vyake. Iwapo unahitaji kula tufaha la baridi, unaruhusiwa kuliweka kwenye jokofu kwa muda usiozidi dakika 30 tu! 

VITUNGUU: Kitunguu maji huwa hakitakiwi kuwekwa kwenye jokofu pia. Chakula au kitoweo kilichoungwa kwa vitunguu vilivyowekwa kwenye jokofu kwa muda mrefu huwa na ladha tofauti na pia harufu ya kitunguu kwenye chakula husikika zaidi kuliko kawaida.

PARACHICHI: Kama ilivyo kwa ndizi mbivu, ndivyo ilivyo kwa parachichi pia. Kulihifadhi parachichi kwenye jokofu ni kulizuia kuendelea kuiva na hivyo kupunguza kiwango cha virutubisho vinavyotakiwa kwenye tunda hilo. 

KAHAWA: Ladha ya kahawa huongezeka inapohifadhiwa kwenye joto la kawaida. Kahawa kabla haijasagwa isihifadhiwe kwenye jokofu kwani ladha yake huharibika na kuwa na ladha tofauti baada ya kuvuta na kunyonya harufu ya vyakula vilivyomo kwenye jokofu. Unaweza kukuta kahawa ina ladha ya nyanya, kitunguu au ndizi iwapo itahifadhiwa kwenye jokofu pamoja na vitu hivyo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.