Monday, August 24, 2015

Anonymous

Dr. Dre Awaomba Radhi WANAWAKE Wote Aliowafanyia UKATILI!

dr-dre-may-be-his-rap-name-but-his-real-name-is-andre-romelle-young
Mmiliki wa Lebo ya Aftermath Entertainment, Andre Romelle ‘Dr Dre’.
New York, Marekani MMILIKI wa Lebo ya Aftermath Entertainment, Andre Romelle ‘Dr Dre’, 50, ameibuka na kuwaomba radhi wanawake wote aliowahi kuwafanyia mambo ya kikatili, akiwemo Michel’le ambaye alizaa naye mtoto mmoja miaka ya 1990.
Dr Dre ambaye alitamba kinomanoma na Ngoma ya I Need a Doctor na Still Dre, ameomba radhi kupitia mahojiano maalum aliyofanya na Jarida la The New York Times wiki iliyopita.Dr Dre aliripotiwa kuwapiga wapenzi wake wa zamani, Tairrie B aliyekuwa naye kwenye lebo moja na Michel’le ambaye kipigo kilisababisha akawa na macho meusi na kumvunja mbavu. 
 
“Ninawaomba radhi wanawake wote niliowafanyia mambo haya ya kikatili, sikuwa na akili ya uelewa lakini sasa nimekua, najitambua kama mwanaume bora.“Nikiwa na miaka 25 nilikuwa bado mdogo na nilikuwa nakunywa sana pombe na kuwafanyia ukatili wanawake wangu, sikuwa na mpangilio wa kimaisha.
“Nimeoa kwa miaka 19 iliyopita, ninajitahidi kuwa mwanaume bora kwenye familia yangu. Ninafanya kila kitu ili nisionekane kama mtu yule tena,” alisema Dr Dre ambaye amemuoa Nicole Young tangu mwaka 1996.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.