Friday, July 24, 2015

Anonymous

SARAFINA YULE WA AFRIKA KUSINI AWAFUNDA MASTAA WANAOTUMIKA KINGONO BONGO!

Staa mwenye jina kubwa duniani kutoka Sauzi, Leleti Khumalo ‘Sarafina’.
Imelda Mtema, Zanzibar
 Staa mwenye jina kubwa duniani kutoka Sauzi, Leleti Khumalo ‘Sarafina’ amewafunda mastaa wa kike kwa kuwataka wajitume ili kujiletea maendeleo kwa kuwa muda wa kutumiwa kingono na wanaume umepita. 

Akizungumza na Ijumaa mjini hapa akiwa mmoja wa wasanii waliohudhuria Tamasha la Ziff, Sarafina aliseme kuwa baadhi ya wasanii wamekuwa wakijiweka nyuma na wakati mwingine kukubali kutumiwa kingono ili watoke wakati uwezo wanao.

“Hapa Afrika waongozaji wa filamu wa kike ni kama hamna wapo wachache sana, wanawake wanahitaji kusimama na kufanya kazi zao wenyewe, muda wa kutumiwa kingono umepita, amkeni mfanye kazi wanawake wenzangu,” alisema Sarafina.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.