Friday, July 24, 2015

Anonymous

SANDRA Akimbia Ukata Bongo Muvi!

salama_h_salmin_sandraMuigizaji Filamu za Bongo, Salama Salimin ‘Sandra’
Brighton Masalu
MUIGIZAJI aliyekuza jina kupitia Filamu ya Misukosuko, Salama Salimin ‘Sandra’ amesema sababu iliyomfanya kukaa kimya kwenye uigizaji ni malipo na kipato kidogo hivyo kuamua kutafuta riziki kwa njia nyingine (hakuzitaja).

Akizungumzia maisha yake kwa sasa, msanii huyo asiye na makuu alisema hamaanishi kazi ya sanaa haina masilahi, isipokuwa kwa upande wake aliona hapati kile alichokihitaji licha ya kuwa na kipaji halisi cha uigizaji.
“Unajua ni lazima uwe na mikakati mingi katika kutafuta maisha, huwezi kung’ang’ana na kitu kimoja tu, kwa upande wangu filamu hazinilipi kama ninavyohitaji, ndiyo maana nikaamua kukaa pembeni kwanza, lakini simaanishi kuwa kazi ya sanaa haina masilahi, la hasha ila ni maoni ya upande wangu,” alisema Sandra.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.