Friday, July 31, 2015

Anonymous

Ne-Yo Aeleza Kwanini Alikuwa na Hamu ya Kuonana na DIAMOND Platnumz Alipoenda Afrika Kusini!

Muimbaji wa Marekani, Shaffer Chimere Smith maarufu kama Ne-Yo ameitaja sababu iliyomfanya atake sana kukutana na Diamond Platnumz.
Baada ya watu kusikia kuwa nilikuwa nakuja kwenye MAMAs jina pekee ambalo walikuwa wakilitaja kwangu ni Diamond Platnumz,” Ne-Yo alimwambia Vanessa Mdee kwenye interview ya MTV Base.

Nikasema ni lazima nikutane na huyu jamaa, nahitaji kumuona,” aliongeza.
Siku moja kabla ya tuzo hizo pia, Diamond alielezea jinsi Ne-Yo alivyomtafuta. “Wakati nazungumza na D’banj @salaam_sk alinifata na kuniambia @neyo anakutafuta anataka kukuona…” Ungependa kujua kilichofata??? Kaa karibu na TV, Radio yaani Kiufupi Media zako Soon utayaskia,” aliandika Diamond kwenye Instagram.
Ne-Yo na Diamond ni miongoni mwa wasanii waliotumbuiza kwenye MTV MAMA 2015.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.