Friday, July 31, 2015

Anonymous

LOWASSA Kwenda UKAWA Sawa Ila Wanasiasa Siyo wa Kuwaamini!


Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akionesha kadi ya Chadema mara baada ya kusajiriwa rasmi na chama hicho.

]HAKUNA adui wala rafiki wa kudumu katika siasa. Huu ni msemo ulioasisiwa na mwanadiplomasia wa Israel, Avil Primor ambaye amepata kufanya kazi katika nchi mbalimbali duniani, ikiwemo ubalozi wa nchi yake nchini Ujerumani (1993-99) na katika Umoja wa Ulaya (1987-91).

LOWASSA Lowaasa akionesha fomu ya kuwania urais kwa tiketi ya Chadema, fomu aliyochukua mapema jana kwenye ofisi za  Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar, jana.

Alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumzia urafiki kati ya nchi yake na Iran ulivyokuwa. Kabla ya mapinduzi ya nchi hiyo ya Kiarabu ambayo ni taifa la Kiislamu mwaka 1979 yaliyomuweka katika himaya Ayatollah Khomeini, wawili hao walikuwa ni marafiki wa kufa mtu. Enzi hizo, Iran ilikuwa ni ardhi pekee kati ya mataifa yote ya Kiarabu, ambayo yaliruhusu ndege za Israel kutua!

10.Lowassa akizungumza jambo.…Akizungumza na umati wakati wa hafla ya kuchukua fomu ya kuwania urais kwa tiketi ya Chadema.

Leo, unapoitaja Iran mbele ya Israel ni sawa na uhai na kifo. Ni maadui ambao kila mmoja anatamani mwenzake ateketee mara moja. Lakini Primor, licha ya kusema hakuna adui wala rafiki wa kudumu katika siasa, aliongeza kuwa kilicho cha kudumu kwa wanasiasa ni masilahi yao!

Hilo ndilo tunalolishuhudia leo baada ya Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Ngoyai Lowassa anapokuwa sehemu ya jeshi la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambacho kwa miaka mingi, kimemtaja kama mmoja wa mafisadi wanaostahili kuogopwa katika nchi hii.

11.Meza kuu,kutoka kushoto,Mke wa Mhe.Edward Lowassa,Regina Lowassa,Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrosia na Maendeleo,Freeman Mbowepamoja na Mgombea Urais kupitia Chama hicho,Edward Lowassa.Mke wa Lowassa, Regina Lowassa (kushoto), Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe (katikati), na Edward Lowassa (kulia).
Mwaka mmoja kabla hajajiuzulu kwa kashfa ya kampuni tata ya kufua umeme ya Richmond, Lowassa alikuwa mmoja wa viongozi 11 waliotajwa na Dk. Willbroad Slaa kuwemo katika orodha ya mafisadi iliyojipatia umaarufu kama List of Shame.

Katika orodha ya watu hao waliotajwa, wapo wengine ambao pia wamehusishwa katika kashfa nyingine zilizohusu uporaji wa mabilioni ya shilingi za umma kwa kutumia nafasi zao za kiuongozi walizopata kuzishikilia siku za nyuma au hadi sasa wakiwa katika ofisi za umma.

Akiwa serikalini, tangu enzi za Rais William Mkapa na sasa Jakaya Kikwete, Lowassa alikuwa mmoja wa viongozi wa juu waliokuwa wakitoa maneno mengi ya kejeli, kashfa na dharau kwa vyama vya upinzani vilipojaribu kwa namna yoyote, kuhatarisha neema za wakubwa wa chama na serikali.

Na Chadema, kimejipatia umaarufu mkubwa kwa jamii ya wanyonge baada ya kuonesha kuwa ni chama chenye nia ya kupambana na ufisadi na kutowajibika kwa viongozi wa umma, kiasi kwamba idadi kubwa ya wafuasi wake ni watu waliokata tamaa na ambao kwa namna moja au nyingine, hawafaidiki moja kwa moja na uwepo wa CCM madarakani.

Uadui wa wawili hawa umemalizika. Leo Chadema wanamtaja Lowassa kama mchapakazi aliyeathiriwa na mfumo wa kifisadi ndani ya CCM na mbunge huyo wa Monduli, anaamini chama chake kipya ndicho pekee kinachoweza kuwaondoa marafiki zake wa siku nyingi madarakani.

Uadui na urafiki unaweza kumalizika wakati wowote, lakini masilahi ya wanasiasa daima huwa ya kudumu. Lengo la Chadema (Ukawa) ni kushika dola, bila kujali inashirikiana na nani na ndivyo pia ilivyo kwa Lowassa, kwamba hamu yake ni kukalia kile kiti cha enzi pale magogoni, bila kujali anafikaje.

Nia yangu hapa ni kujaribu kuwaweka sawa wafuatiliaji wa safu hii, kama nilivyopata kuwapa dokezo wiki iliyopita kuwa wanatakiwa kuwa macho sana na wanasiasa kwa sababu hawaaminiki.

Wanachokisema hakitoki ndani ya mioyo yao, isipokuwa kinatokana na wakati wenye kuhusisha masilahi yao.

Kwa kuwa Lowassa ana watu wengi nyuma yake wanaoweza kuwasaidia Ukawa wakaingia Ikulu, hawana shida kuungana naye, hata kama miongoni mwao, watakuwa ni walewale waliotajwa Septemba ile, pale uwanja wa Mwembeyanga, mwaka 2007.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.