Baada ya muigizaji mrembo wa filamu za Bongo, Elizabeth “Lulu”
Michael kuandika tweet iliyotafsiriwa kuwa huenda ni kijembe kwa
mrembo fulani, amefafanua alichokimaanisha.
Lulu amesema kuwa alichokiandika kwenye post hiyo ilikuwa ni utani,
na wakati huo huo kukubali kuwa inaweza kuwa na ukweli ndani yake.
KISA MAGUFULI KUCHAGULIWA KUIWAKILISHA CCM URAIS 2015
“It was a joke, but sort of ukweli pia kwa sababu mara nyingi
kumekuwa na dhana watu wa nje wanachukulia kama vile viti maalum ni vya
kupeana” alisema kupitia The Playlist ya Times Fm.
Hiki ndicho alipost:
Lulu aliendelea kwa kusema:
“…probably watu wameichukulia kama nimemsnitch mtu, mimi siko
hivyo na sinaga hayo mambo kabisa. Ni kwamba nimefanya kama utani,
lakini watu wasichukulie poa kwamba kila anaewekwa pale kwamba ana sura
nzuri, kila anaewekwa pale ana umbo zuri.”

Note: Only a member of this blog may post a comment.