Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe,
amesema utitiri wa wagombea urais kupitia CCM kunaonyesha dalili ya wao
wenyewe kutoaminiana, kutothaminiana na kimepoteza hazina ya viongozi.
Aidha, alisema kazi ya urais ingekuwa
inachukuliwa kwa uzito wagombea wa CCM wasingefikia 10 badala yake
imeonekana ni kazi nyepesi na imerahisishwa na CCM. Kabwe alisema sifa
13 pekee za wagombea wa CCM ni nyepesi ndio maana kila mmoja anajiona
anaweza kuwa kiongozi wa nchi.
Kabwe alisema moja ya sifa ya chama cha
ACT-Wazalendo ni wagombea kufuata masharti kwa kutangaza mali na madeni
ikiwamo kufuata miiko ya viongozi iliyotangazwa na Azimio la Tabora.
Kabwe aliwataja viongozi hao kuwa ni wa kitaifa wa chama, rais, mawaziri, wabunge na madiwani watakaotokana na chama hicho.
Aliongeza kuwa ili kubomoa mfumo wa
kinyonyaji na kifisadi miongoni mwa viongozi, chama hicho kimeamua
kurejesha miiko ya uongozi na kuishia ambayo imehusishwa kutokana na
Azimio la Arusha.
“Chama
kinamtaka kiongozi katika uongozi wa umma asiwe mkurugenzi katika
kampuni au shirika la umma, awe wazi na vyanzo vyake vya mapato, mali
alizonazo kwa kuzingatia utaratibu wa sheria ya nchi na kanuni za
mwenendo na maadili ya viongozi,” Kabwe.
Pia, alisema kiongozi anatakiwa asiwe mfanyabiashara wa aina yoyote katika chama na serikali anapokuwa kwenye nafasi ya uongozi.
Alisema tangu wagombea hao waanze
kutangaza nia hakuna mgombea urais aliyetamka neno miiko isipokuwa
Samuel Sitta pekee, licha ya kuahidi kupambana na rushwa pamoja na
ufisadi.
“Nitolee
mfano nchi ya Canada, Uingereza, Marekani wana miiko lakini Tanzania
tunageuza uongozi kuwa kichaka cha wezi kwa kutupa miiko pembeni,”Kabwe.


Note: Only a member of this blog may post a comment.