Sunday, June 21, 2015

Anonymous

UKAWA: Tunamsubiri Kwa Hamu EDWARD LOWASSA!

Wakati idadi ya makada wa CCM waliochukua fomu ikifikia 38 jana, UKAWA wanajipanga  kumkabili LOWASSA . 
Ukawa inamuona Lowassa kama ndiye mgombea kutoka CCM  ambaye ndiye wanaweza kukabiliana naye katika uchaguzi mkuu ujao kutokana na jina lake kuvuma sana hasa wakati huu mwana siasa huyo pamoja na makada wengine wa CCM wakizungumza Mikoani kuomba udhamini. 

Mwenyekiti wa CHADEMA, Mbowe alisema wanamsubiri kwa hamu Lowassa katika kinyang’anyiro cha Urais katika uchaguzi wa mwaka huu. 

Katika mkutano uliofanyika kwenye viwanja wa njoro, Moshi, Mbowe aliwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapigakura pamoja na kufanya mabadiliko katika uchaguzi mkuu ujao. 

Amesema ameona watu wengi wakimpamba Lowassa ambaye ametangaza nia ya kugombea Urais kupitia CCM, hivyo wanansubiri amalize michakato yote kwenye chama chake aje kukutana na Ukawa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.