Wakati idadi ya makada wa CCM waliochukua fomu ikifikia 38 jana, UKAWA wanajipanga kumkabili LOWASSA .
Ukawa inamuona Lowassa kama ndiye
mgombea kutoka CCM ambaye ndiye wanaweza kukabiliana naye katika
uchaguzi mkuu ujao kutokana na jina lake kuvuma sana hasa wakati huu
mwana siasa huyo pamoja na makada wengine wa CCM wakizungumza Mikoani
kuomba udhamini.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Mbowe alisema wanamsubiri kwa hamu Lowassa katika kinyang’anyiro cha Urais katika uchaguzi wa mwaka huu.
Katika mkutano uliofanyika kwenye
viwanja wa njoro, Moshi, Mbowe aliwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi
kujiandikisha katika daftari la wapigakura pamoja na kufanya mabadiliko
katika uchaguzi mkuu ujao.
Amesema ameona watu wengi wakimpamba
Lowassa ambaye ametangaza nia ya kugombea Urais kupitia CCM, hivyo
wanansubiri amalize michakato yote kwenye chama chake aje kukutana na
Ukawa.


Note: Only a member of this blog may post a comment.