Wakati
fainali ya Champions League kwa mwaka 2016 ilipotangazwa itachezwa
katika dimba la San Siro, mashabiki wa vilabu vya AC Milan na Inter
Milan vinavyotumia uwanja huo kwa mechi walianza kuwa na ndoto za kupata
ufalme wa soka barani ulaya katika uwanja wao wa nyumbani.
Ni Real Madrid pekee, ambao wameshinda ubingwa wa ulaya mara nyingi
kuliko AC Milan, wakati miaka 5 iliyopita Inter Milan walitwaa ubingwa
huo.
Lakini wakati vigogo viwili vya soka barani ulaya vitakuwa
vikiutafuta ubingwa wa ulaya jijini Milan Mei 2016, hakutakuwa na nafasi
ya wenyeji wa mji huo kupata uwakilishi kwenye michuano hiyo.
Inter Milan imemaliza ligi ikiwa nafasi ya 8, huku AC Milan ikiwa nafasi ya 10.

Note: Only a member of this blog may post a comment.