Tuesday, May 26, 2015

Anonymous

Kingine alichokisema Lowassa leo! Majimbo kuongezeka Dar? Rais yupi anatakiwa TZ 2015? #PowerBreakfast (Audio)

May 26 2015 siasa zimeendelea kutawala kwenye Headlines kwenye kurasa za Magazeti TZ.
Iko stori ya Baraza la Madiwani Manispaa ya Kinondoni limependekeza kuongezeka kwa Majimbo ya Uchaguzi Wilaya ya Kinondoni, Rais JK amemteua Mkuu mpya wa Wilaya na wengine 10 kuwabadilisha vituo vyao vya kazi.. nyingine inahusu Rais JK kuwaonya vijana wa CCM walio vyuoni kuacha kutumiwa kama makuwadi. 

Askari wawili Rukwa wanashikiliwa kutokana na upotevu wa SMG kwenye kituo cha Polisi, Mzee Cleopa Msuya amesema TZ inahitaji Rais dikteta.. stori nyingine inahusu mrembo mwenye asili ya India kugombanisha matajiri wawili Dar ambao walizidiana dau, UKAWA wamesema wakipita kwenye Urais 2015 watapitisha Serikali ya mseto, Waziri Membe amesema atatangaza nia yake kugombea Urais akiwa Kijijini kwao. 

Kasikika pia Mbunge Edward Lowassa akizungumzia tatizo la ajira TZ na elimu, stori zote ziko kwenye hii sauti hapa kutoka #PowerBreakfast @CloudsFM.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.