Monday, May 18, 2015

Anonymous

HARUNA NIYONZIMA Amwagiwa Mamilioni YANGA SC na Kuchukua Uamuzi Huu!

Nicodemus Jonas na Sweetbert Lukonge Dar es Salaam
BAADA ya kuzingua kwa muda mrefu, hatimaye nyota wa Yanga, Haruna Niyonzima, raia wa Rwanda, amekubali kumwaga wino Jangwani kwa dau la Sh milioni 70 za usajili huku mshahara wake ukiwa Sh milioni tano kwa mwezi, ambao ukiupigia mahesabu kwa mwaka, atakuwa akichukua jumla ya Sh milioni 60.

Katika mkataba wake uliomalizika, Niyonzima alikuwa analipwa Sh milioni nne kwa mwezi lakini Yanga wameamua kumuongezea robo ya mshahara wake huo ili amwage wino.Ukiachana na Niyonzima, nyota mwingine raia wa Rwanda, Mbuyu Twite naye hatimaye amesaini Yanga.

Nyota hao ambao wamekuwa viungo muhimu klabuni hapo kwa misimu mitatu mfululizo, hivi karibuni walikuwa wakihusishwa kutaka kuondoka Jangwani kutokana na mikataba yao kufika kikomo baada ya kumalizika kwa ligi kuu msimu huu.

Mbuyu alikuwa akitajwa kuhitajika nchini Kenya na Tunisia lakini kwa Niyonzima ilikuwa tofauti, alikuwa akidengua kusaini mkataba mpya akitaka cha juu zaidi, lakini suala hilo rasmi limefutwa baada ya nyota hao kumwaga wino juzi na jana.
Habari za uhakika ndani ya Yanga zilizolifikia Championi Jumatatu ni kwamba, Mbuyu amepewa mkataba wa mwaka mmoja wakati Niyonzima amekubali kubaki kwa kupewa miaka miwili, pia akiongezwa mshahara kwa asilimia kadhaa.

“Mbuyu tumemalizana naye tangu jana (juzi Jumamosi), tumeamua kumpa mkataba wa mwaka mmoja tu, kikubwa tumezingatia kigezo cha umri (inatajwa ana miaka 34), kwa hiyo kumpa muda mrefu tunaweza kujikuta tunaingia hasara.
“Niyonzima yeye amekubali kuendelea klabuni na leo (jana) tumemalizana naye. Kikubwa ni kwamba kilichokuwa kinakwamisha ni suala la maslahi lakini tunashukuru katika hilo tumeelewana,” kilisema chanzo hicho cha habari na kuongeza:

“Kikwazo kikubwa katika usajili wa Niyonzima kilikuwa ni juu ya mshahara, hivyo ili kuondoa malumbano, ilibidi tumpandishie robo ya ule wa awali.”Aliposakwa Niyonzima, hakuwa tayari kuweka wazi suala hilo lakini alionyesha kushtushwa sana. “Nani kakwambia jambo hilo? Bado sijasaini ila muda ukifika kila kitu kitakuwa wazi.

“Kwa sasa nipo bize na familia yangu, hivyo sipendi kujihusisha na mambo mengine, kwani muda wa usajili bado ni mrefu na Yanga wanalijua hilo,” alisema Niyonzima.Katika hatua nyingine chanzo hicho kiliongeza kuwa, mchezaji mwingine kati ya nane waliokuwa wamemaliza mikataba yao klabuni hapo, kipa Deogratius Munishi “Dida’, naye ameongeza mkataba wa miaka miwili.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.