Monday, May 18, 2015

Anonymous

MUSSA MGOSI afumua kikosi SIMBA SC

Wilbert Molandi,Dar es Salaam
MSHAMBULIAJI mkongwe wa zamani wa Simba, Mussa Mgosi, amekifumua kikosi cha timu hiyo kwa kutoa mapendekezo ya kusajili wachezaji watatu.

Mgosi ametoa kauli hiyo baada ya Simba kushindwa kutwaa taji la Ligi Kuu Bara kwa mwaka wa tatu sasa.

Mshambuliaji huyo anayeichezea Mtibwa Sugar, aliiwezesha Simba kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara mwaka 2010 huku akiibuka mfungaji bora kwa kufunga mabao 18, lakini baadaye aliiacha timu hiyo na kutimkia DC Motema Pembe ya DR Congo kabla ya kurudi Bongo. 

Akizungumza na Championi Jumatatu, Mgosi alisema kuwa kati ya nafasi ambazo Simba wanatakiwa kuziboresha ni safu ya ulinzi ya kati, kiungo na ushambuliaji.Mgosi ambaye aliwafunga Simba katika mchezo wa mzunguko wa kwanza Morogoro, walipokutana msimu uliopita wa ligi kuu, alisema safu ya ulinzi ni butu inayohitajika kuimarishwa ili kuhakikisha hawaruhusu mabao. 

Aliongeza kuwa, pia timu hiyo inatakiwa kusajili mshambuliaji mmoja mwenye uwezo mkubwa wa kufunga mabao baada ya kumuacha kimakosa Mrundi, Amissi Tambwe.“Ni ukweli ulio wazi kabisa, viongozi wa Simba walikosea kumuacha Tambwe ambaye msimu uliopita alikuwa mfungaji bora na kumsajili Sserunkuma (Danny). 

“Hapo ndipo Simba walipokosea hesabu zao za ubingwa msimu huu uliomalizika, hivyo wanatakiwa kusajili mshambuliaji mwingine mwenye uwezo mkubwa wa kufunga mabao.“Pia wasajili kiungo mmoja atakayemchezesha mshambuliaji huyo mpya watakayemsajili, pia wanatakiwa kusajili mabeki wawili wa kati wenye uwezo mkubwa,” alisema Mgosi.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.