Wednesday, April 8, 2015

Anonymous

Wauaji wa Albino kupigwa risasi, madereva kugoma na taasisi za fedha kufanya kazi saa 24?…#PowerBreakfast


21958234_BG1
Nimekusogezea hapa miongoni mwa zile habari zilizopewa Headlines kwenye Magazeti ya leo April 8, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Malawi, ameamuru kupigwa risasi mtu atakaekutwa akimuwinda mtu mwenye ulemavu wa ngozi, madereva Tz, wanapanga kufanya mgomo siku ya Ijumaa, SUMATRA yashindwa kutangaza viwango vipya vya nauli kama ilivyoagizwa, utata wagubika kifo cha Askari aliyejiua kwa kujipiga risasi Tabora. 

Wadau wa bandari wamezitaka taasisi za fedha kufanya kazi saa 24, ili kuongeza ufanisi, wakazi wa Mwenge waiomba Serikali kuwapatia huduma ya kituo cha abiria, radi nyingine yaua watu 3, huko Geita, muumini aliyeingia na bastola Kanisani aachiliwa kwa dhamana na Askofu asema anatamani kumpiga Waziri kwa kushindwa kuzuia malori yanayoharibu barabara.
Bonyeza play hapa chini kusikiliza uchambuzi wa story zote za leo…
-via millardayo

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.