Monday, April 27, 2015

Anonymous

VIDEO: Mwanaume Amteketeza Mpenziwe Kwa Moto na Kujijeruhi Huko Kericho, Kenya!

Nimefikiwa na hii story kutoka Kenya,  inahusu mgogoro wa mapenzi kati ya mwanaume na mwanamke.. chanzo cha ugomvi hakijafahamika, jamaa alifika kwenye duka hilo, wakajibizana na mwanamke huyo, mwisho wa mzozo jamaa akammwagia mwanamke petrol, akajimwagia na yeye mwenyewe  alafu akawasha moto ambao uliteketeza  jengo la gorofa lililopo Kericho. 

Mwanamke huyo alifariki hapohapo, huyo jamaa alipata majeraha makubwa pamoja na watu wengine wanne walijeruhiwa pia..“Akaanza kuwasukuma wateja waliokuwa katika M-Pesa akawaambia wacha nihudumiwe ndio akawasha kiberiti“, alisema shuhuda mmoja aliyekuwa eneo hilo pia. 

Maduka yaliyopo kwenye jengo hilo yaliwaka moto, ikabidi vikosi vya zimamoto kufika ili kuuzima moto huo ambao tayari ulikuwa umeathiri sehemu kubwa ya jengo hilo.

Hii ishu ilikuwa kubwa sana, unaweza kuona hapa hali ilivyokuwa baada ya moto huo kuwashwa..

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.