Vinara wa ligi kuu Engaland wanakutana na wababe wengine wa ligi hiyo Arsenal mwishoni mwa juma hili katika uwanja wa Emirates ikiwa ni harakati za kuwania ubingwa wa ligi hiyo.
Lakini kauli ya mashabiki wa Arsenal kwa nahodha wao wa zamani Cesc Fabregas ambaye kwa sasa anaichezea Chelsea inaweza kukuchekesha kwani wameutaka uongozi wa klabu hiyo kuondoa bango lenye picha ya staa huyo kwenye uwanja wao.
Mashabiki hao wamesisitizan lazima bango
hilo liondolewe kabla ya mchezo wao Jumapili kwa kuwa Fabregas anarudi
kwenye uwanja huo akiwa mpinzani wao mkubwa.
Fabregas raia wa Hispania aliichezea
Arsenal kwa mafanikio makubwa kabla ya kuondoka mwaka 2011 na kujiunga
na Barcelona lakini akarejea England na kujiunga na Chelsea ambayo sasa
inapambana na Arsenal katika kuwania ubingwa wa Ligi Kuu England Jumapili hii.

Note: Only a member of this blog may post a comment.