POWERBREAKFAST
ya Clouds FM imefanya uchambuzi wa story kubwa zote za kwenye kurasa za
Magazeti Tz, kama ulikuwa mbali na Redio yako basi unaweza kusoma na
kusikiliza stori zote zilizosikika hewani leo April 07, hapa.
April 07, ni sikukuu ya KARUME DAY ikiwa ni kumbukumbu ya kifo cha aliyekuwa Rais wa kwanza Zanzibar, Abeid Amani Karume,
Mwenyekiti wa jumuia ya wafanyabiashara amesema hakuna dalili za
viongozi waliopo madarakani kumaliza mgogoro uliopo kati ya
wafanyabiashara na TRA, Mkurugenzi wa taasisi ya Mw. Nyerere, Joseph Butiku amesema mambo ya msingi yaliyotolewa kwenye Katiba mpya yarejeshwe, Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa
amesema haelewi ni kwa nini Serikali imeshindwa kuteketeza meno ya
Tembo na wagonjwa wanaolazwa katika Hoptitali ya Wilaya ya Kondoa
wanalazimishwa kufanya usafi wodini.
Magaidi watumia mbinu ya kuwapa mafunzo
wananchi wa nchi husika ili kurahisisha kupanua mtandao wao, mashine
248, za BVR zimewasili nchini kwa ajili ya zoezi la kuandikisha wapiga
kura, Maaskofu wa Japani wamponya Askofu Gwajima
kwa maombi maalumu, wananchi wafanya uharibifu katika treni mpya ya
kisasa ya Delux, watu watano wamefariki baada ya kupigwa na radi wakiwa
Kanisani huko Geita, waumini wa Kanisa Katoliki jimbo la Mpanda
walishindwa kusali baada ya kutokea ugomvi wa kwaya mbili za Kanisa
hilo.
Bonyeza play hapa chini kusikiliza story zote…
-via millardayo

Note: Only a member of this blog may post a comment.