Saturday, April 11, 2015

Anonymous

Hiki ndio kingine alichofanya Cristiano Ronaldo usiku huu! #LaLIga

  
Ligi kuu ya Hispania imeendelea tena jioni ya leo – huku Real Madrid na Elbar wakifungua pazia la mechi za leo.
Mwanasoka bora wa dunia, Cristiano Ronaldo  ameziteka tena ‘headlines’ za vyombo vya habari baada ya leo kuiongoza timu yake kupata ushindi wa magoli 3-0Ronaldo alifungua akaunti yake ya magoli leo kwa mkwaju wa adhabu ndogo katika dakika ya 21 ya mchezo huo – goli la leo limemfanya Ronaldo atimize magoli 38 katika La Liga msimu huu. 
 Goli hilo lilotokana na mkwaju wa adhabu ndogo ni la kwanza tangu Ronaldo alipofunga goli dhidi ya Bayern Munich katika nusu fainali ya Champions League takribani miezi 12 iliyopita.
Magoli mengine ya mchezo huo yalifungwa na Javier Hernandez Chicharito dakika ya 31 na Jesse akamalizia kazi kwa goli zuri dakika ya 83.
FC Barcelona wanaongoza ligi ya Spain wanacheza na Sevilla usiku huu.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.