DUNIA IMEKWISHA: ASHITAKIWA KWA KUMTIA MIMBA BINTIYE
MAHAKAMA
moja mjini Bungoma nchini Kenya imemshtaki ofisa mmoja wa wadi ya
Bukembe kwa kulala na mwanawe wa kike mwenye umri wa miaka 14 kwa zaidi
ya miaka miwili baada ya mkewe kufariki mwaka 2013.
Kulingana na gazeti la The Standard nchini Kenya, mwathiriwa ambaye
ni mjamzito wa miezi minne amesema kuwa mshukiwa huyo ambaye ni babaake
amekuwa akimlazimisha kufanya mapenzi naye kila usiku na kumuonya kwamba
angemdhuru iwapo angemwambia mtu yeyote.
''Babaangu pia ameninyima fursa ya kwenda sekondari licha ya mimi
kufanya vyema katika mtihani wa KCPE. Mwaka 2013,nilifanya vyema lakini
akanilazimisha kurudia darasa. Mwaka jana nilifanya vizuri zaidi lakini
anadhani kwamba iwapo nitajiunga na shule ya bweni, nitamkosesha fursa
ya kufanya tendo la ngono name, '' mwathiriwa aliiambia mahakama.
Hakimu mwandamizi, Peter Irer,i alimwachilia mtuhumiwa kwa dhamana ya shilingi 100,000 ama pesa taslimu shilingi 20,000.
CHANZO: BBC SWAHILI
USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK
TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)
Note: Only a member of this blog may post a comment.