Wednesday, April 8, 2015

Anonymous

Diamond azidi kung'ara! Atajwa kuwania tuzo ya ‘Radio AFRO Australia Song of the Year 2014’...Maelezo zaidi yapo hapa!

remix number 1
Hit song ya Diamond Platnumz iliyomfungulia milango mingi ya kimataifa ‘Number 1 Remix’ aliyomshirikisha staa wa Nigeria Davido, umetajwa kuwania tuzo ya ‘Radio AFRO Australia Song of the Year 2014’.

Wasanii wengine kutoka Afrika wanaowania Tuzo hizo ni pamoja na Davido ambaye ana nyimbo nne zilizoingia, Bebe Cool ana nyimbo mbili, P-Square wana nyimbo nne. Wengine ni 2Face, AKA, Cassper Nyovest, Iyanya.
Tuzo hizi hufanyika kila mwaka na wasikilizaji wa Afro Radio ya Australia hupiga kura mtandanoni na msanii atakayepata kura nyingi ndiye anaibuka mshindi.
Afro Australia Awards
Ili kumpigia kura Diamond na kumfanya ashinde bonyeza hapa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.