Moja ya magari yanayotumiwa na chama cha ACT Tanzania baada ya kugonga na kusababisha kifo cha mtu mmoja.
Kamanda wa Polisi Mkoani Tabora Susan Kaganda
alisema gari hilo lilikuwa linaendesha na mmoja wa madereva
anayejulikana kwa jina la Mabona Kabwe lilikuwa likitokea Nzega kwenda
Tabora mjini.
Alipofika eneo la Magiri lilimgonga
mwanamke mmoja aliyekuwa akivuka barabara baada ya kushuka kwenye gari
alilokuwa amepanda akiwa na mtoto wake wa miezi 10 ambaye aliumia vibaya
na kufariki dunia wakati akitibiwa.
“Gari hilo lilikuwa kwenye mwendo kazi na haikuwa rahisi kuweza kumkwepa mama huyo na kumgonga hapo hapo” Kaganda.
Hata hivyo mama huyo amehamishwa hospitali ya Kitete kwa matibabu zaidi.


Note: Only a member of this blog may post a comment.