Watu wengi wanaotumia mitandao kama
Instagram ni wapenzi wa pichaz, hasa vijana yani time zote utakuta tu
wanapost picha zao wakishare na marafiki zao basi inakuwa poa.
Sasa sio kila sehemu unaruhusiwa kuingia
na selfie stick kwa ajili ya kujiselfie, Majumba ya Maonesho ya sanaa
Uingereza wamepiga marufuku mtu yoyote kuingia na selfie stick ndani ya
majumba hayo.
Uamuzi wa kuzuia mtu yoyote kutumia
selfie stick unatokana na mapendekezo yaliyotolewa na watu wanaosimamia
Nyumba za Sanaa za Maonesho.. wanasema watu wanaoingia na selfie stick
na kupiga picha wanawazuia watu wengine kuenjoy kuangalia picha na vitu
mbalimbali vilivyomo ndani ya majumba hayo, vilevile sio salama sana kwa
picha ambazo zinaning’inizwa kwenye majumba hayo.
Uingereza sio wa kwanza kuzuia selfie
stick, Marekani pia walitangaza kuzuia matumizi ya vifaa hivyo kwenye
Majumba ya Makumbusho.. Arsenal ilizuia mtu yoyote kuingia uwanja wa Emirates wakati wa mechi kwa kuwa kifaa hicho wanakichukulia kama silaha nyingine tu kwa hiyo ni hatari kama mtu akiingia nayo uwanjani.
Manchester United nao walizuia, Tottenham Hotspurs nao walitangaza kwamba watazuia mtu yoyote kuingia kwenye Uwanja wao wa White Hart Lane na selfie stick.
Korea Kusini walienda mbali zaidi, mpango wao ilikuwa ni kuzuia kabisa selfie stick..
-millardayo



Note: Only a member of this blog may post a comment.