Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA)
limethibitisha tarehe ya kufanyika kwa fainali za michuano ya kimataifa
ya Kombe la Dunia ambazo zitakazofanyika nchini Qatar.
FIFA imeweka hadharani tarehe ya fainali hizo wakati wa kikao chake jana huko Zurich, Switzerland ambapo
itakuwa Desemba 18, 2022 huku ikisisitiza tarehe hiyo lakini Uingereza
wameanza kulalamika wakidai ratiba hiyo mpya itavuruga ratiba ya ligi
yao.
Kawaida kombe la dunia hufanyika kati ya
mwezi June na July lakini hali ya hewa ya Qatar imesababisha
kubadilishwa kwa ratiba hiyo.

Note: Only a member of this blog may post a comment.