Kazi hiyo mpya inayoandaliwa na mtayarishaji mkongwe, John Mahundi akishirikana Marco Chali, inasimamiwa na AY.
“Yeah mzigo upo jikoni na soon utausikia maskioni,” GK ameiambia Bongo5. “Sidhani kama itaathiri kutoka kwa kazi za East Coast ila inawezekana kwa sababu huwezi kuachia kazi mbili kwa pamoja, lazima moja ianze kwanza na nyingine ifuate,” ameongeza.
“Beat kila kitu kimeandaliwa na John Mahundi na Vanessa ndo anaingiza vocals kwa Marco Chali. Kiukweli hii kazi imesimamiwa kila kitu na AY na baada ya hapo hii project itatoka.”
GK amesema anamshirikisha Vanessa kwa kuwa ni muimbaji wa kike anayemkubali zaidi.
“Unajua Vanessa ni hatari sana kwenye muziki, ana uwezo mzuri sana ndio maana ukamuona kwenye hii project yetu.”
Vifurushi vipya vya mitandao [8MB]: TCRA yatoa tamko na maagizo kwa makampuni ya simu!
===>>SOMA ZAIDI HAPA!
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU
UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.
===>>SOMA ZAIDI HAPA!
ASANTE NA KARIBU
TENA!


Note: Only a member of this blog may post a comment.