Kuna time utakuwa unajiuliza maswali kuwa kuna umuhimu gani kwa wasanii wa hapa Tanzania kufanya kolabo na mastaa wa Afrika.
Sasa staa wa Bongo Fleva Ali Kiba amejibu swali lako na kusema;‘Katika kutangaza muziki inasaidia kiasi fulani lakini sio sana, muziki unaweza ukautangaza hata wewe mwenyewe, mimi binafsi muziki wangu nimeutangaza mbali sidhani kama Afrika hainijui bali inanifahamu sema tu kiukweli video zangu nilizokuwa nafanya hazikuwa katika quality nzuri huo ni ukweli naujua kwa hiyo sasa hivi tuko vizuri katika kujipanga nahakikisha kila kitu kitakuwa poa, hiyo inasaidia sana vile vile kubadilisha muziki na kuutangaza muziki wako katika msanii yoyote ambaye umemchukua labda wa Congo, Nigeria, Uganda, sehemu nyingine nyingi ili watu waweza kukusikiliza kwa urahisi na vile vile ni support kubwa inaonesha jinsi gani una ushirikiano na watu wengine‘-Alisema.
JIUNGE
NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU
UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU
TENA
Note: Only a member of this blog may post a comment.