Bondia Mtanzania Francis Cheka ambaye mwishoni mwa wiki alipoteza pambano lake nchini India alilopigana na raia wa nchi hiyo Vijender Singh, ameibuka na kusema kuwa mpinzani wake huyo hakumpiga, ila alibebwa na mwamuzi.
“Tatizo nilikuwa nakohoa, nilijiandaa vizuri kumpiga yule Vijender,” alisema Cheka.
Pia katika mtandao wake wa Instagram aliandika:
Pale ambapo matokeo yamepangwa, tunaenda kukamilisha ratiba tu, Refa unaona mouth guard imetoka na unaendelea kuchezesha… Watanzania nadhani mmeona, tusiwage wanyonge kwao na kwetu pia… Nadhani nimeliwakilisha taifa vyema, kuitangaza Morogoro, Tanzania, Kiswahili na Kimakonde pia.


Note: Only a member of this blog may post a comment.