Thursday, September 15, 2016

Unknown

Habari Mbaya Kwa Mashabiki Wa Manchester United

Beki wa klabu ya Manchester United, Phil Jones anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa muda wa mwezi mmoja kutokana na matatizo ya goti aliyoyapata akiwa mazoezini.

Kocha wa timu hiyo Jose Mourinho amethibitisha kuhusu tatizo hilo na kusema kuwa uchunguzi unaendelea.
Jones amekuwa akiandamwa na majeraha ya mara kwa mara na ni mchezaji ambaye amekuwa na uwezo wa kucheza kama beki wa kati, pembeni na mara kadhaa kama kiungo mkabaji.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.