Monday, March 7, 2016

Anonymous

Kama Ulifikiwa na Taarifa za Uhaba wa Sukari Chukua Hii...


Issue ya uhaba wa sukari ilichukua headline baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania John Pombe Magufuli kupiga marufuku uingizaji wa sukari kutoka mataifa ya kigeni ili kuvilinda viwanda vya sukari nchini ambavyo vimeathiriwa na uingizaji na uagizaji wa sukari ya bei rahisi kutoka nje.

Kuzuiwa kwa sukari ya nje ikasemekana kumesababisha tatizo la mfumuko wa bei ya sukari licha ya kuzalishwa kwa wingi hapa nchini. Leo March 7 2016 Waziri wa Viwanda na Biashara Charles Mwijage amezungumzia hilo wakati akijibu maswali ya wanahabari na kukanusha kuwepo kwa uhaba wa sukari nchini….
>>> ‘Hakuna uhaba wa sukari, kuna sukari ya kutosha na ambaye anaficha hiyo sukari yake kwanza nimeshaagiza tena nije nimtafute mkurugenzi wa leseni kama kuna godown lina leseni nikalifunge godown tuone huyo anayeficha sukari‘:-Charles Mwijage 

>>>’kwa hiyo hakuna uhaba wa sukari kama kuna mtu anajua kuna mtu anaficha sukari aje aniambie, mimi naweza kufunga godown la mtu yeyote hapa nchini simuogopi mtu yeyote kwa hiyo hakuna uhaba, uhaba unatengenezwa,  mimi nafanya survey nauliza sukari inauzwa bei gani kwenye maeneo mbalimbali nchini‘:-Charles Mwijage 

Awali Waziri huyo amezungumzia ujio wa Rais wa Vietnam, Truong Tan Sang, huku akibainisha umuhimu wa ujio wa Rais huyo hasa katika kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya watu, Waziri Mwijage ameelezea lengo la ujio huo…
tujifunze kwa hawa watu ambao walikuwa kama sisi, lakini sasa hivi wako mbali sana, ukiangalia takwimu zetu za biashara, tofauti ya kiasi tunachoagiza kwao na tunachonunua tuna tofauti ya dola milioni 49, lakini tunapenda washirika wetu hawa wanunue zaidi kwetu na sisi tununue zaidi kwao lakini zaidi ni namna wanavyofanya kazi‘:-Charles Mwijage

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.