Imekuwa kawaida kwa watu kubishana kuhusu wachezaji bora wa Dunia ambao wote wamewahi kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Dunia Ballon d’Or kwa zaidi ya mara moja Lionel Messi na Cristiano Ronaldo kuwa yupi ni bora zaidi ya mwenzie.
Hii mada ambayo mara nyingi haijawahi
kupatiwa majibu yaani kwa upande fulani, kuridhika na kukiri kuwa fulani
ni bora hususani kwa mashabiki wa pande zote mbili, stori kubwa March 7
iliyoingia kwenye headlines ni kuhusu kifo cha jamaa aliyekuwa
anabishana kuhusu Ronaldo na Messi nani bora.
Obina Durumchukwu mwenye umri wa miaka 34 ameuawa na mnigeria mwenzake, Michael Chukwuma mwenye umri wa miaka 21 kwa kuchomwa na chupa iliyopasuka, kisa ni kubishana nae kuwa nani bora kati ya Messi na Ronaldo. Mabishano hayo yalitokea Mumbai India wakiwa katika party.
Note: Only a member of this blog may post a comment.