Aliyekuwa shabiki namba moja wa muigizaji wema sepetu(Team wema) , matilda au maarufu kama matikibokoyao ametoboa moja ya siri ya aliyekua boss wake kuwa huwa anakopa nguo kwa mfanyabiashara maarufu mjini aitwaye manyota, hivyo amemtaka msanii huyo mpenda kick mjini aende akalipe madeni ya watu.
Akiendelea kumwaga ubuyu, Yuda huyo hakumuacha nyuma muigizaji lulu michael na kudai kuwa na yeye pia ana madeni sugu kama ilivyo kwa boss wake(Wema).
Bifu hilo liliendelea mbele zaidi ambapo shabiki huyo wa madame aliapa kutoboa siri kibao za boss wake huyo , hata hivyo baadae madame baada ya kuona mambo yake yanaanza kuanikwa alianza kujirudi taratibu kwa mfuasi wake huyo na kuyamaliza kiutu uzima
Chanzo: Jamii Forums


Note: Only a member of this blog may post a comment.