Serikali imefanikiwa kukusanya zaidi ya
shilingi trilioni moja kwa mwezi huu tofauti na zilizokuwa zikukusanya
hapo awali za bilioni 850 kwa kipindi cha mwezi mmoja na kuzielekeza
fedha hizo kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo.
Takwimu hizo zimetolewa leo jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile wakati akitoa taarifa ya hali ya mapato kwa kipindi cha mwezi Februari mwaka huu.
Likwelile amesema ‘kati
ya fedha hizo ,sekta ya elimu imepewa shilingi bilioni 18.7 kwa ajili
ya utekelezaji wa utoaji wa elimu bure kwa wanafunzi wa shule za awali
hadi kidato cha Nne ambapo fedha hizo ni kwa ajili ya malipo ya
ada,chakula pamoja na ruzuku‘.
‘Mkoa wa Dar es salaam imeongezewa
shilingi bilioni 2 ili kupanua uwezo wa udahili kama Rais alivyoahidi
katika mkutano wake na Wazee wa Mkoa huo na kati ya fedha hizo
wakufunzi wamepatiwa shilingi milioni 431.6 walimu walio masomoni
wametengewa shilingi milioni 249.2 kwa ajili ya vifaa vya kufundishia,
posho na nauli‘
‘ fedha nyingine kati ya hizo kiasi cha shilingi bilioni 573.7
zimetolewa kwa ajili ya mishahara ya watumishi wa Umma , ulipaji wa
deni la taifa kwa mwezi huu zimetolewa shilingi bilioni 842.1 na Mifuko
ya hifadhi za Jamii zimetolewa shilingi bilioni 81.13‘
Unaweza kumtazama hapa Katibu Mkuu Dkt. Servacius Likwelile


Note: Only a member of this blog may post a comment.