Saturday, February 27, 2016

Anonymous

Sijui Kama WEMA SEPETU Alishawahi Kuwa na Mimba -Mirror


Msanii wa muziki wa bongo fleva Mirror, anayefanya kazi chini ya Wema Sepetu amesema hajui kama Wema alishawahi kuwa na mimba ila na yeye anasikia kwa watu na kwenye mitandao.

Msanii huyo ambaye anatamba na wimbo wake mpya Naogopa ambao ameimba na Baraka Da Prince ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano katika kipindi cha ENews kinachorushwa na EATV.
 Mirror amesema hafahamu chochote kuhusiana na jambo hilo na wiki 2 zilizopita nilikuwa naye ofisini lakini sikuona kama kuna tatizo lolote yupo ana furaha na anaendelea na kazi zake kama kawaida .
Ikumbukwe kuwa hivi karibuni Idriss Sultan alinukuliwa akisema watoto wake mapacha ambao walikuwa wapatikane kupitia Wema haikuwa bahati,kuwaona.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.