Tuesday, February 23, 2016

Anonymous

RAY C Aeleza Jinsi Magazeti ya Udaku Yanavyomliza Mama Yake

Rehema Chalamila ‘Ray C’ amesema mama yake amekuwa akipatwa na presha mara kwa mara kutokana na habari anazo ziona kwenye magazeti ya udaku kuwa mwanae amerudia matumizi ya madawa ya kulevya.
Akizungumza katika kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Television, Ray C amesema mama yake hana amani kutokana na mambo yanayo andikwa kwenye magazeti ya udaku.
“Mimi naweza nikasema nakushtaki, wewe una hela zaidi na unaweza ukanishinda, your powerful get a gun watu wanifyatue na wampige mama yangu, maana mama yangu yupo hospitali ana presha kwa sababu ya gazeti yake,” alisema Ray.
Wiki chache zilizopita gazeti la Ijumaa liliandika habari kuwa mwanadada huyo alionekama mazingira fulani ambayo yanadaiwa kupatikana madawa ya kulevya.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.